MASHINDANO YA MISS WOLRD TANZANIA YASHINDWA NG'ARA .....


@nkupamah blog

.

SANYA,China

Kwa mara nyingine tena, mrembo wa Tanzania ameshindwa kunga’ara katika mashindano ya mrembo wa
Dunia. Katika fainali zilizofanyika jana mrembo wa Tanzania, Lilian Kamazima, hakuambulia chochote.
Mshindi wa Miss World 2015 ni binti mwenye miaka 23 toka Hispania ,Mireia Lalaguna Royo. Nafasi ya pili iliwenda kwa Mrusi , Sofia Nikitchuk wakati nafasi ya tatu ilikwenda Indonesia ambayo iliwakilishwa na mrembo Maria Harfanti.Mireia-Lalaguna-Rozo
Siku mbili zilizopita zilisambaa taarifa katika mitandao ya kijamii kwamba Lilian Kamazima amefika kumi bora, lakini taarifa hizo si za kweli. kumi bora katika michuano hii ilihusisha warembo toka mataifa ya Urusi,
Ufilipino, Guyana, Lebanon, Hispania, Afrika ya Kusini,Ufaransa, Australia , Jamaica na Indonesia.
Tangu mrembo Nancy Sumari aweke rekodi ya kuwa Miss World Africa, hakuna mrembo aliewahi kuifikia rekodi hiyo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment