Nkupamah media
Serikali imewaonya wadau wa elimu nchini
wanaoendelea kutoza wanafunzi fedha za kwa ajili ya kujisajili pamoja
na michango mbalimbali waache mara moja.
Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa
Elimu,Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhandisi Stella Manyanya alipokuwa
akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu agizo la elimu bila malipo kwa
Shule zote za Umma pamoja na mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu.
“ Napenda kusisitiza kuwa Wakuu wa Wilaya na
Wakurugenzi wa Halmashauri ,Miji na Manispaa zote nchini wafuatilie kwa
karibu utekelezaji wa agizo hilo na watoe taarifa za Walimu Wakuu na
Wakuu wa Shule watakaokwenda kinyume ili hatua stahiki zichukuliwe”
Alisema Mhandisi Manyanya.
Pia Mhandisi Manyanya ameitaka jamii kutoa
ushirikiano kwa kutoa taarifa katika Ofisi za Elimu zilizopo katika
maeneo yao pale wanapobaini kuwa kuna shule zinakiuka agizo hilo.
Akijibu swali kuhusu suala la ada elekezi
Kamishna wa Elimu Prof Eustella Bhalalusesa alisema kuwa ataitisha kikao
na wamiliki wa shule binafsi kujadili kuhusu utozaji wa ada ambazo
zitakuwa na unafuu kwa wananchi
.
Aidha Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Elimu ya
Juu Bw. Jonathan .S. Mbwamba amesisitiza kuwa kila mwanafunzi mwenye
sifa atapata mkopo na kuongeza kuwa idadi ya wanafuzi wanaopata mkopo
imefikia wanafunzi 53,032 kutoka kwenye lengo lililowekwa la kuwapatia
mkopo wanafunzi 13,582.
Kuanzia mwaka wa masomo 2016, elimu katika
shule za Umma itatolewa bure kupitia Waraka namba 5 wa mwaka 2015 kuhusu
utoaji wa elimu pasipo malipo na Waraka namba 6 wa mwaka 2015 ambao
ulitoa ufafanuzi na melekezo ya utekelezaji wake
0 comments :
Post a Comment