Wataalam kutoka Wizara za Nishati
na Madini,Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ,Wizara ya maji, na
Umwagiliaji , Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco )pamoja na Watalamu wa
bonde la mto Rufiji walitembelea vyanzo vya maji vinavyotiririsha maji
katika mito mikubwa inayomwaga maji
katika mabwawa ya kuzalisha umeme
wa maji ya Mtera, Kihansi na Kidatu ili kuangalia uharibifu wa vyanzo
hivyo vya maji na kuchukua hatua za kuzuia uharibifu huo
Wataalam hao waliunganisha nguvu
ya pamoja ili kurejesha utunzaji na usalama wa vyanzo hivyo ili viwe
katika hali yake ya awali kutokana na kuathiriwa na shughuli za
kibinadamu zinazoendelea na kusababisha kukauka kwa maji na kusababisha
upungufu mkubwa katika mabwawa ya kuzalisha umeme tofauti na ilivyokuwa
katika miaka ya nyuma.
Muonekano wa Bwawa la Kihansi kwa
sasa ambalo pia limepunguza uzalishaji wa umeme wa maji kutokana na
kupungua kwa kina cha maji.
Timu ya wataalamu kutoka Wizara
ya Nishati na Madini,Wizara ya kilimo, mifugo na uvuvi ,Wizara ya maji,
na umwagiliaji , Shirika l Umeme Tanzania (Tanesco )pamoja na Watalamu
wa bonde la mto Rufiji waliotembelea vyanzo vya maji vinavyotiririsha
maji katika Mabwawa ya kuzalisha umeme wakiendelea na ukaguzi wao .
Eneo lenye chanzo cha cha maji
pamoja cha mto Mbalo mto huu hutumiwa kwa shughuli za kibinadamu na
kusababisha upotevu wa maji yanayoingia katika katika mabwawa ya
kuzalisha umeme wa maji
Moja ya sehemu ya mashine ama mtambo inayotumika kuzalisha umeme wa maji katika vituo vya Kihansi, Kitadu na Mtera.
Mashine inayotumika kuondoa taka kama vile magogo na nyingine za
namna hiyo katika mabwawa ya kuzalisha umeme wa maji.
namna hiyo katika mabwawa ya kuzalisha umeme wa maji.
Baadhi ya wajumbe wa Timu ya
kutoka Wizara ya Nishati na Madini,Wizara ya kilimo, mifugo na uvuvi
,Wizara ya maji, na umwagiliaji , Shirika l Umeme Tanzania (Tanesco
)pamoja na Watalamu wa bonde la mto Rufiji wakipata maelezo ya namna
ambavyo umeme wa maji huzalishwa katika kituo cha Kihansi .


0 comments :
Post a Comment