Cheka ashinda, mpinzani wake adai amebebwa.

Nkupamah media:

Francis Cheka
Francis Cheka ametwaa Mkanda wa Ngumi wa Ubingwa wa Mabara baada ya kumkung'uta kwa pointi mpinzani wake, Geard Ajetovic kutoka Serbia, ambaye hata hivyo aliukataa ushindi huo wa bondia kutoka Mji Kasoro Bahari akidai alibebwa na majaji.
Pambano hilo la uzito wa kati linalotambuliwa na Shirikisho la Ngumi Duniani (WBF), lilifanyika usiku wa kuamkia jana jijini Dar es Salaam.
Majaji watatu Anthony Lutta, Sako Mtulya na Ibrahim Kamwe wote kutoka Tanzania, walimpa ushindi Cheka wa pointi 115-112, 115-112 na 116-111.
Baada ya pambano Cheka alisema kuwa ushindi wake haukuwa rahisi kwa vile mpinzani wake alikuwa mkali na kutumia nguvu nyingi.
"Ajetovic alitamba angenipiga kwa KO, lakini ilikuwa ngumu kwangu kutokana na kujiandaa vizuri," alisema Cheka.
Lakini mambo yalikuwa tofauti kwa mpinzani wake, Ajetovic aliyegoma kuzungumza na waandishi wa habari akidai majaji 'walimpa' ushindi Cheka.
Katika mapambano ya utangulizi Cosmas Cheka alimpiga Mustapha Dotto kwa pointi na kufanikiwa kutwaa ubingwa wa WBF Afrika, huku Mohamed Matumla akimdunda Bakari Mohamed na Seleman Zugo akimshinda kwa pointi Mwinyi Mzengela na Mwanne Haji alimdunda Lulu Kayage katika pambano la mabondia wanawake.
Abdallah Pazi alimpiga kwa KO raundi ya nne Baraka Mwansope, huku Mohamed Amir akimshindilia makonde Yusuph  Kombo na kuibuka mshindi kwa pointi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment