Yanga yafuata 'kizizi' cha Azam FC Pemba.

Nkupamah media:


   Timu hiyo ya Jangwani imelazimika kurejea Pemba ilikonasa mbinu zilizoipa ushindi dhidi ya Simba katika mechi mbili zilizopita.
 
Jerry Muro, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Yanga.
Baada ya kufanikiwa kuifunga Simba katika mechi zote mbili za msimu huu, kikosi cha Yanga kimekimbilia tena Pemba kuweka kambi maalum kabla ya kuikabili Azam FC kwenye Uwanja wa Taifa Jumamosi.
 
Katika miaka ya karibuni, timu hiyo ya Jangwani imeachana na utaratibu wake wa kupiga kambi Bagamoyo mkoani Pwani kabla ya kucheza mechi kubwa na badala yake imekuwa ikijichimbia visiwani Zanzibar.
 
Katika kile kinachoonekana kambi ya Pemba inalipa, mabingwa hao mara 25 wa Tanzania Bara, wamefanikiwa kufunga mabao 4-0 katika mechi mbili zilizopita dhidi ya watani wao wa jadi, Simba.
 
Na ili kufanya vyema Jumamosi dhidi ya wapinzani wao wakubwa kwenye mbio za ubingwa msimu huu, Azam FC, kikosi cha Mdachi Hans van der Pluijm kiliondoka jijini Dar es Salaam jana mchana kwenda Pemba kikipaa kwa 'pipa' la kukodi.
 
Kwa mujibu wa Jerry Muro, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Yanga, nyota 23 na watendaji wengine wote wa benchi lao la ufundi walikwea pipa jana kwenda Pemba kusaka dozi ya Wanalambalamba.
 
"Tumeamua kwenda na wachezaji wote 24, lakini waliosafiri leo (jana) ni 23, (Donald) Ngoma bado hajarejea nchini (kutoka kwao Zimbabwe)," Muro alisema.
 
"Tunatarajia atarejea nchini leo (jana) mchana au kesho (leo). Pemba kuna utulivu na uwanja wa kapeti kwa ajili ya mazoezi. Ndiyo maana tunapapenda kwa kambi za timu yetu."
 
Yanga wanaongoza msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara wakiwa na mtaji wa pointi 46 baada ya mechi 19 sawa na Azam FC, lakini mabingwa watetezi wapo kileleni kwa wastani mzuri wa mabao.
 
Mechi ya Jumamosi inatarajiwa kutoa taswira halisi ya timu itakayokuwa na nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa wa msimu huu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment