KilimoJoint: Suluhisho kwa vijana na jamii ya wapenda kilimo na ufugaji wa samaki nchini


Miongoni mwa mambo ambayo yanachangia vijana wengi kukaa vijiweni na hata kujiingiza katika makundi mabaya ni pamoja na uvivu. Ili kuendana na kauli ya ‘Hapa Kazi Tu’  wadau wa masuala ya Kilimo hapa nchini, KolimoJoint wao wamekuja na mkakati kabambe wa kuwainua vijana katika kufikia malengo yao hasa katika suala la kilimo.
“Hapa Kazi Tu’, Ni kauli mbiu aliyokuja nayo mheshimiwa rais wa awamu ya tano Tanzania Dk. John Magufuli Pombe ambayo nasi kama ‪#‎KilimoJointtunapenda kuituma ili mkulima mdogo hususani kijana aweze kujikwamua katika maisha kwa kujiajiri kwa kupitia kilimo na ufugaji” wanaelezea KilimoJoint.
Miongoni mwa huduma wanazotoa ni pamoja na ushauri na usambazaji wa-Umwagiliaji wa njia ya matone, Mbegu, kitalu nyumba, Mafunzo na ufuatiliaji,Insect nets,Solaring covers, Ufugaji wa samaki, Kapeti za kuhifadhia maji,Chakula cha samaki  na mambo mbalimbali yanayohusu Kilimo.
Ilikumsaidia kijana kufikia malengo yake, pia waweza kuwasiliana n KilimoJoint kupitia  barua pepe kilimojoint@gmail.com au kupitia kurasa yao ya mtandao wa kijamii wa facebook.
“Kilimo cha kisasa sio uchafu”.
kilimojoint2Pichani baadhi ya vijana wakipata elimu ya ujasiriamali wa Kilimo ambao ni muhimu kabla hujajikita kwenye kilimo biashara. Tambua soko lako linauhitaji gani muda huo, mazao yapi yanastawi zaidi kwenye eneo ulilopo? Mbolea gani utumie Kwa aina ya udongo wako. Mbegu ya aina gani na je ni zile zilizoboreshwa au?. (Picha zote kwa hisani ya mtandao wa KilimoJoint).
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment