 
 TAARIFA KWA UMMA
UAMUZI WA BODI YA WAKURUGENZI YA MCC WA KUSITISHA MAHUSIANO NA TANZANIA YATAWAUMIZA WANANCHI WA VIJIJINI
CHAMA
 cha ACT-Wazalendo kimeupokea kwa masikitiko makubwa uamuzi wa Bodi ya 
Wakurugenzi wa wa MCC wa kusisitisha mahusiano na Tanzania.
MCC
 ni Shirika la misaada la Marekani lilianzishwa na Bunge la Nchi hiyo 
mwaka 2004 kwa lengo la kusaidia miradi ya maendeleo katika nchi 
mbalimbali duniani kwa ajili ya kuchochea ukuaji wa haraka wa uchumi.
Tangu
 kuanzishwa kwake, shirika hili limesaidia miradi mingi ya maendeleo 
nchini ikiwemo ujenzi wa barabarani na usambazaji wa umeme vijijini kwa 
sasa miradi ya aina hiyo inaendelea sehemu mbali mbali hapa nchini na 
miongoni mwao ni pamoja na mradi wa REA,miradi ya barabara kama ile ya 
Tnduma Sumbawanga pamoja na Tanga katika barabara ya Horohoro.
Pamoja
 na vigezo vingine, kigezo mama kwa nchi kufuzu kupata misaada ya MCC ni
 kwa nchi husika kuzingatia misingi kidemokrasia ikiwemo kufanya 
uchaguzi ulio huru na haki.
Jana
 tarehe 28 Machi 2016 Shirika la MCC lilitangaza kusitisha mahusiano na 
Tanzania kutokana na serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM),kubariki 
kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi wa Zanzibar uliofanyika tarehe 25 Oktoba
 205 na kubariki kurudiwa kwa uchaguzi huo tarehe 20 Machi 2016 katika 
mazingira ambayo hayakuzingatia misingi ya demokrasia ya vyama vingi na 
kuvunja matunda ya mwafaka wa kisiasa na kikatiba uliojengwa kwa gharama
 kubwa visiwani humo.
Chama
 cha ACT-Wazalendo kinapigania nchi yetu kujitegemea kiuchumi kama 
msingi wa kujenga utu na uhuru endelevu wa kisiasa na kijamii. Hata 
hivyo tunatambua kwamba katika kipindi hiki nchi yetu inahitaji 
mahusiano mema na Jumuiya ya Kimataifa na wadau mbalimbali wa maendeleo 
duniani, likiwemo shirika la MCC, katika kuendeleza miradi ya maendeleo.
 Shirika la MCC limekuwa mdau mkubwa katika miradi ya barabara na 
kusambaza umeme vijini.
Uamuzi huu wa Bodi ya Wakurugenzi wa MCC utawaumiza na kukwaza juhudi za wananchi wa vijijini katika kujikwamua na umaskini.
Tunasikitika
 kwamba ubabe wa Serikali ya CCM na woga wake wa kushindana kidemokrasia
 umesababisha nchi yetu ikose pesa za MCC ambazo zingesukuma mbele 
juhudi za kupambana na umaskini.
Tunatoa
 wito tena kwa Serikali ya chama cha Mapinduzi kuacha ubabe na kufifisha
 juhudi za miaka ishirini za ujenzi wa demokrasia hapa nchini. Tunatoa 
wito maalumu kwa wadau wote wa siasa visiwani Zanzibar kurudi mezani na 
kutatua mgogoro wa kisiasa kwa njia za kistaraabu na katika hali ambayo 
itarudisha heshima ya nchi yetu katika kukuza demokrasia nchini.
Imetolewa na
Theopister Kumwenda
Makamu Mwenyekiti, Kamati ya Katiba, Sheria na Mambo ya Nje
29/03/2016


0 comments :
Post a Comment