Mgombea Urais Kupitia Chama Cha Republican Teddy Cruz Ajitoa......... Marekani


Teddy Cruz wa chama cha Republican
Seneta wa jimbo la Texas Ted Cruz amejiondoa katika kinyanganyiro cha uteuzi kugombea nafasi ya urais wa Marekani kupitia chama cha Republican.
Alitoa tangazo lake punde tu baada ya kupoteza kura katika kampeni za mwisho Indiana.Cruz amewaambia wafuasi wake kuwa alifanya kila analoweza katika kampeni zake,lakini hakukuwa na njia ya yeye kuweza kusonga mbele zaidi.
Mwandishi wa BBC aliyepo katika vituo vya kupigia kura Indiana amesema wafuasi wa Cruz wamestushwa na kukatishwa tamaa.Tangazo hilo linatoa mwanya kwa Donald Trump kupata uteuzi wa chama chake cha Republican. 
Chanzo:BBC
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment