Msimu
wa 2015/2016 umemalizika vizuri kwa Barcelona baada ya hapo usiku wa
kuamkia leo Jumatatu kushinda Kombe la Copa Del Rey bbaada ya kuipa
kichapo cha goli 2-0 klabu ya Sevilla katika mchezo wa fainali.
Magoli
yaliyowapa Barcelona ubingwa yalifungwa na Jordi Alba katika dakika ya
97 baada ya dakika 90 kumalizika bila kufungana na mwamuzi Carlos del
Cerro kuongeza dakika 30 za muda wa ziada na goli la pili likifungwa na
Mbrazil, Neymar.
Aidha
timu zote zilimaliza mchezo huo wa fainali zikiwa na wachezaji nusu
baada ya Mascherano kwa upande wa Barcelona kuonyeshwa kadi nyekudu
dakika ya 36 na upande wa Sevilla wachezaji wake Ever Banega dk. 90 na
Daniel Carrico katika dakika ya 120.
Ubingwa huo kwa Barcelona umekuwa wa pili kwa msimu huu baada ya kushinda kobe la Ligi Kuu ya Hispania(La Liga).
Blogger Comment
Facebook Comment