Kesi
namba 208 ya mwaka 2016 ya gazeti la Mawio imeaghirishwa hadi Oktoba 4,
2016 baada ya mshitakiwa namba moja Tundu Lissu kutohudhuria mahakamani
kwa ajili ya kusikiliza shitaka.
Awali,
wadhamini wa Lissu Ibrahim Ahmed na Robert Katula walisimama mbele ya
Hakimu Thomas Simba anayesimamia kesi hiyo, na kusema kuwa Lissu
hakutokea leo mahakamani kwa sababu amesafiri nje ya nchi kwa ajili ya
matibabu.
Hata
hivyo, upande wa mashitaka ukiongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali
Mutalemwa Kisheruji uliiomba mahakama kuzuia hati ya kusafiria ya
mshitakiwa Lissu pamoja na kumuwekea sharti la kuiomba mahakama kibali
cha kusafiria endapo atarudia tena kosa hilo kutokana kwamba hakufuata
sheria kwa sababu alitakiwa kutoa taarifa mapema kabla ya siku ya shtaka
kusikilizwa.
Lakini
Hoja hiyo ilipingwa na Wakili wa upande wa utetezi Peter Kibatala na
kuiomba mahakama kutenga siku nyingine ambapo alimuahidi hakimu kuwa
kosa hilo halitajirudia tena na siku husika ya kusikilizwa shitaka
mshatikiwa atakuja mahakamani.
Baada
ya kusikiliza maombi ya pande zote mbili, Hakimu Simba alitoa onyo kali
kwa mshitakiwa na kuwaambia wadhamini wa Lissu kuwa, endapo siku nyingi
mshitakiwa huyo hatakuja mahakamani, wadhamini watalipa dhamana.
Hakimu
Simba ameiaghirisha kesi hiyo hadi Oktoba, 4, 2016 baada ya mawakili wa
pande zote mbili kuiridhia tarehe hiyo iwe siku ya kusikilizwa shtaka
hilo.


0 comments :
Post a Comment