Mchezaji
na kocha wa zamani wa Simba, Abdallah King Kibaden amefunguka kuhusu
uwekezaji ambao Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa Makampuni ya Mohammed
Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group), Mohammed Dewji anataka
kuufanya katika klabu ya Simba kwa kununua hisa asilimia 51 kwa kitita
cha Bilioni 20 za kitanzania.
Akizungumza
katika kipindi cha Sports Xtra cha Clouds Fm, Kibaden alisema mchezo wa
soka unahitaji pesa nyingi ili kufanikiwa na kama MO Dewji ana nia ya
dhati kuwekeza pesa kwa ajili ya kuisaidia Simba basi yeye anakubaliana
na jambo hilo.
“Pesa
ni muhimu kwenye soka, kila kitu kinahitaji pesa, maana hata wachezaji
wanalipwa, kuna vitu vingi vinahitaji pesa, inabidi wapatikane watu wa
kutusaidia ili tuwe kwenye biashara maana mpira ni biashara na lazima
kupata watu sahihi wa kufanya nao biashara, pesa inahitajika ili
kufanikiwa,
“Kuwepo
na matajiri sio tatizo, tunataka biashara ya kuleta maendeleo, mimi
kama MO anataka kuwekeza nabariki kuchukua Simba na sio hata MO peke
yake, kama kuna watu wengine watajitokeza ambao watataka kuwekeza
wanaweza kujitokeza na kuwekeza,” alisema Kibaden.


0 comments :
Post a Comment