MAWAZIRI
wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu kutoka nchi mbalimbali za kiafrika,
wanachama wa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF,
wamekutana Jijini Washington DC, Marekan,i na kuzitaka Taasisi hizo
kuweka mipango inayoakisi na kutatua changamoto zinazolikabili bara hilo
ikiwemo, uhalifu, umasikini, mizozo ya kivita na majanga yanayotokana
na mabadiliko ya tabia nchi
Aidha,
Viongozi hao wamezitaka taasisi hizo kuweka uwiano wa uwakilishi wa
uongozi wa juu ili kuhakikisha kuwa maslahi mapana ya nchi hizo
yanalindwa na maendeleo endelevu yanafikiwa kwa haraka.
Akizungumza
kwenye moja ya mikutano hiyo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip
Mpango, ambaye kiutaratibu ni mmoja wa Magavana wa Benki ya Dunia na
IMF, amesema kuwa mashirika hayo ya fedha ya kimataifa yanamchango
mkubwa kwa maendeleo ya nchi za kiafrika ikiwemo Tanzania.
Waziri
wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akiwa na Waziri wa Fedha wa
Swaziland kushoto kwake walipokuwa kwenye mkutano na Mkurugenzi
Mtendaji Bi. Christine Lagarde Jijini washington DC- Marekani.
Hata
hivyo amesema kuwa mdororo wa uchumi duniani, ambao unaonesha kuwa
viwango vya ukuaji wa uchumi vilivyokadiriwa kufikiwa kwa asilimia 3,
havitafikiwa ambapo takwimu zinaonesha kuwa ukuaji wake hivi sasa ni
asilimia 1.5 tu, unaashiria namna nchi wanachama zinatakiwa kujipanga
kuhakikisha kuwa uchumi unapanda.
Dkt.
Mpango amesema kuwa uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi kwa wastani wa
asilimia 7 kwa mwaka lakini changamoto kubwa iliyopo ni kuhakikisha kuwa
uchumi huo unaonekana katika maisha ya kawaida ya wananchi wake
“Kila
mara utasikia malalamiko ya wananchi kwamba uchumi wetu unakua kwa
namba tu hawaoni ni kwa kiasi gani uchumi huo wanauona katika maisha yao
ya kawaida kwa hiyo ili uchumi uhesabike kuwa unakua ni lazima uwe
jumuishi na ushirikishe watu wengi” alisema Dkt. Mpango.
Wajumbe
wa Tanzania waliohudhuria mkutano wa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha
Duniani-IMF, wakimsikiliza kwa makini Rais wa Benki ya Dunia Dkt. Jim
Yong Kim (hayupo pichani) wakati Mawaziri wa Fedha na makatibu wakuu
(Magavana) kutoka nchi wanachama wa Taasisi hizo kutoka Bara la Afrika,
walipokutana kama kamati, Jijini Washington DC, Marekani.
Amesema
kuwa hali hiyo itawezekana ikiwa sekta zinazochangia maendeleo kwa kasi
zaidi kama kilimo, uvuvi, biashara ya miamala ya simu, miundombinu na
viwanda, zitaimarishwa ili kukuza ajira na kuongeza kipato cha wananchi.
“Tunataka
kilimo kiwe cha kisasa na cha kibiashara kwa kutumia zana na pembejeo
bora za kilimo, uongezaji wa thamani ya mazao na kuwa na masoko ya
uhakika ili kukuza ajira nyingi hususani kwa vijana” Aliongeza Dkt.
Mpango.
Amebainisha
kuwa Tanzania itaendeleza uhusiano mzuri uliopo kati yake na Benki ya
Dunia na Shirika la Fedha Duniani-IMF na kuwataka watanzania waelewe
kuwa mikopo na ruzuku zinazotafutwa na serikali yao ni kwaajili ya
kuwaletea maendeleo kwa kuwekeza kwenye miradi yenye tija.
Benny Mwaipaja, MoFP-Washington DC, Marekani
Waziri
wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akiwa na Katibu Mkuu Bw. Dotto
James (kulia) wakiandika pointi muhimu wakati Rais wa Benki ya Dunia,
Dkt. Jim Yong Kim, alipowahutubia Mawaziri wa Fedha na Makatibu wakuu
(Magavana) kutoka nchi za Kiafrika wanaoshiriki Mkutano wa Mwaka wa
Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani-IMF, Jijini Washington
DC-Marekani.
Waziri
wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akiwa na Katibu Mkuu wa wizara
ya Fedha Bw. Dotto James katika kikao cha Mawaziri wa Fedha na makatibu
Wakuu (Magavana) kutoka nchi za Afrika walipokutana na Rais wa Benki ya
Dunia Dkt. Jim Yong Kim kujadili fursa na changamoto zinazolikabili
Bara la Afrika kiuchumi, kisiasa na kijamii, Jijini Washington DC-
Marekani.
Waziri
wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akiwa na Naibu Gavana wa Benki
Kuu ya Tanzania (BoT) Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, wakibadilishana mawazo
kabla ya kukutana na uongozi wa Juu wa Shirika la Fedha Duniani-IMF,
Kanda ya Afrika, Jijini Washington DC nchini Marekani.
Waziri
wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akisalimiana na Gavana
wa Benki Kuu ya Kenya Bw. Patrick Ngugi Njoroge alipokutana nae kwenye
mikutano ya Benki ya Dunia Jijini Washington DC- Marekani.
Waziri
wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, akifafanua jambo alipokutana na
kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha
Duniani-IMF, Kanda ya Afrika, Bi. Chileshe Mpundu Kapwepwe Hayupo
pichani), Jijini Washington DC-Marekani. Kushoto kwake ni Gavana wa
Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Prof. Benno Ndulu akifuatiwa na Naibu Gavana
wa Benki hiyo Dkt. Natu Mwamba.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Shirika la Fedha Duniani –IMF, Kanda ya Afrika Kundi la
Kwanza, Chileshe Mpundu Kapwepwe (katikati), akisisitiza jambo wakati
alipokutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na
Waziri wa Fedha na Mipango, alipokutana na Ujumbe huo Ofisini kwake
Jijini Washington DC, Marekani.
Gavana
wa Benki Kuu ya Tanzania Prof. Benno Ndulu (aliyenyoosha mkono)
akielezea jambo wakati Ujumbe wa Tanzania Ukiongozwa na Waziri wa Fedha
na Mipango, Dkt. Philip Mpango, kulia kwake, walipokutana na kufanya
mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa IMF Africa Group I Bw. Abebe Aemro
Selassie (Hayupo pichani) ambapo Gavana alieleza kuhusu uchumi wa sasa
wa Tanzania pamoja na Hali ya uchumi unavyokua kwa kiasi cha
kuridhisha, Jijini Washington Marekani.
Makamu
wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Japan-JICA, Hiroshi (Hiro) Kato,
akimwonesha Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Kitabu
Chenye maelezo mbalimbali ya miradi inayotekelezwa nchini Tanzania kwa
ufadhili wa shirika hilo, ambapo Japani imeahidi kuendelea kuwekeza
kiasi kikubwa cha fedha kuendeleza miundombinu ya barabara na sekta ya
kilimo cha umwagiliaji.
Waziri
wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya
Fedha na Mipango Bw. Dotto James (kushoto) wakimsikiliza kwa makini
Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Japan-JICA, Hiroshi (Hiro)
Kato, wakati Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Fedha na Mipango
ulipokutana na Mkurugenzi huyo ambaye ameahidi kuwa Japan itaendelea
kushirikiana na Tanzania katika Nyanja mbalimbali za kiuchumi na
kijamii, Jijini Washington DC, Marekani.
0 comments :
Post a Comment