Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan jana aliongoza
viongozi na wananchi katika mapokezi ya Mwili wa Spika Mstaafu Samuel
Sitta katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere
Jijini Dar es Salaam ukitokea nchini Ujerumani alipofariki wakati
anapatiwa matibabu.
Akizungumzia jinsi anavyomfahamu Samuel Sitta katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan alisema Taifa limeondokewa kiongozi mwadilifu,mzalendo, mchapakazi na mtetezi wa wanyonge hivyo taifa litaendelea kuumuenzi utendaji wake.
Viongozi
mbalimbali waliojumuika na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Samia Suluhu Hassan katika mapokezi ya mwili wa Spika Mstaafu
Samweli Sitta kweye Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Julius Nyerere ni
pamoja na Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Seif Ali
Iddi, Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika, Kikanda na
Kimataifa Dkt Augustine Mahiga na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul
Makonda.
Baada ya Mwili wa Spika Mstaafu Samuel Sitta kuwasili nchini jana mchana alipelekwa nyumbani kwake Masaki jijini Dar es Salaam ambapo leo asubuhi viongozi na wananchi watatoa heshima zao ya mwisho za kuuaga mwili wa marehemu katika viwanja wa Karimjee jijini.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akimpokea mjane wa Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Waziri Mwandamizi Mstafu Marehemu Samuel Sitta, Mama
Margaret Sitta (kushoto) mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege
wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akiwaongoza viongozi mbali mbali wakati wa mapokezi ya mwili wa Spika
Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mwandamizi
Mstafu Marehemu Samuel Sitta







0 comments :
Post a Comment