Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa
atamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli katika mkutano wa kimataifa wa Usafirishaji Duniani
utakaofanyika katika mji wa Ashgabat nchini Turkemistan kuanzia tarehe
26-27 Novemba, 2016.
Ajenda
kuu ya mkutano huo ulioitishwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambao
utashirikisha viongozi mbalimbali utajadili kwa kina maeneo muhimu ya
ushirikiano wa kimataifa kwenye Sekta ya Usafirishaji kwa maendeleo
endelevu Duniani.
Aidha
katika mkutano huo Waziri Prof. Mbarawa atapata fursa ya kukutana na
wawekezaji mbalimbali Duniani waliobobea katika sekta ya usafirishaji na
kuwashawishi kuwekeza hapa nchini.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.



0 comments :
Post a Comment