NA BEATRICE LYIMO-MAELEZO
Chama cha mpira wa Kikapu Dar es 
salaam (RBA) kimeanzaa mashindano ya ligi ya mpira huo 
yatakayoshirikisha timu 16 kutoka kwa wananume na timu nane za wanawake.
Akizungumza na waandishi wa habari
 leo jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa chama hicho Okare Emesu alisema 
kuwa ligi hiyo inatarajiwa kuanza Januari 28 mpaka julai 30  mwaka huu.
Alisema kuwa viongozi wa RBA 
wamekuja na mikakati hiyo ili kuleta chachu kwenye maeneo mengine ya 
mkoa, ligi ya watoto chini ya miaka 14, ligi ya daraja la kwanza, ligi 
ya vyuo, ligi ya mashirika, ligi ya mashule, program maalumu kwa ajili 
ya kukuza vipaji kwa mpira wa kikapu nchini.
“Tangu kuanzishwa kwa chama hiki, 
kumekuwa na mafanikio ya muda mfupi ikiwemo ushiriki kwenye mashindano 
ya Taifa na kushika nafasi ya pili kwa wanaume na wanawake jambo ambalo 
halikuweza kufanyika kwa takribani miaka mitatu sasa” Alisema Mwenyekiti
 huyo.
Aidha akizungumzia kuhusu mfumo wa
 ligi utakaotumika kwenye mashindano hayo, Mkurugenzi wa Mawasiliano na 
Masoko RBA Peter Mpangala alisema kuwa mfumo utakaotumika ni mfumo wa 
nyumbani na ugenini katika hatua za awali na timu nane za wananume za 
nafasi za juu zitacheza mtoano hadi kupata bingwa.
Mbali na hayo alisema kuwa 
kutakuwa na maonyesho ya awali ya ligi ya RBA (Pre RBA Show case) siku 
ya Mapinduzi januari 12, mwaka huu kwenye viwanja vya mpira wa kikapu 
vya Gymkhana yakilenga kukaribisha wadau mbalinmbali kuona mfano wa ligi
 ya RBA itakavyokuwa.
Timu zinazotarajiwa kushiriki 
kwenye ligi hiyo kwa upande wa wanaume ni JKT, Mgulani, Ukonga Kings, 
Magereza, Savio, Pazi, DB Youngstars, Magnet, ABC, Mabibo Bullets, 
Outsiders, Kurasini heat, Oilers, Vijana, Chui na Jogoo na kwa upande wa
 wanawake ni JKT Stars Jeshi  Stars, Vijana Queens, DonBosco Lioness, 
Ukonga Queens, Kurasini Divas na Oilers Princess.


0 comments :
Post a Comment