Timu ya Simba imekoleza mbio za
ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania baada ya kuifanyia mauaji
Majimaji kwa kuifunga goli 3-0 Mchezo uliochezwa uwanja wa Majimaji
Mjini Songea mkoani Ruvuma.
Alikuwa Ibrahim Ajibu Migomba aliwanyanyua mashabiki wa Simba dakika ya 19 akifunga bao kwa kichwa akimalizia pasi ya Shiza Kichuya hadi Mapumziko Simba walikuwa mbele.
Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko hata hivyo Simba waliweza kunufaika na mabadiliko hayo Said Ndemla alifunga bao la pili kwa Mkwaju Mkali dakika ya 64 na kumuacha mlinda mlango wa Majimaji hana la kufanya.
Dakika ya 88 Laudit Mavugo
aliandika kalamu ya magoli kwa kufunga bao safi hadi mwamuzi anamaliza
Mpira Simba wameibuka na pointi tatu na kuendelea kushika nafasi ya
pili.
Kwa Matokeo hayo Simba wamefikisha
Pointi 48 nyumba ya Yanga wenye pointi 49 Ligi hiyo inatarajia
kuendelea kesho kwa Timu ya Azam Fc kucheza na Ndanda kwenye dimba la
Azam Complex Chamazi nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.
0 comments :
Post a Comment