AJALI:Jengo refu zaidi duniani lawaka moto Dubai

Moto mkubwa umelichoma mojawapo ya jumba refu duniani Torch Tower huko Dubai UAE kwa mara ya pili katika kipindi cha miaka miwili.
Picha zilizowekwa katika mitandao ya kijamii zilionyesha moto huo ukisambaa hadi katika jumba hilo huku vifusi vilivyokuwa vikichomeka vikianguka.
Mamlaka baadaye ilisema kuwa wafanyikazi walifanikiwa kuwaondoa watu na wakafanikiwa kuudhibiti moto huo.
Haijulikani ni nini kilichosababisha moto huo katika mojawapo ya jumba refu dunaini.
Hakuna majeraha yoyote yalioripotiwa kufikia sasa katika jumba hilo la Torch Tower ,kulingana na mamlaka ya Dubai iliotuma ujumbe katika Twitter.
Jumba hilo la Torch Tower liliharibiwa na moto mwengine 2015.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment