Mamlaka nchini Sri Lanka zimemkamata mwanamume ambaye alijaribu kusafirisha dhahabu na vito vya karibu kilo moja, alivyokwa ameficha sehemu ya nyuma ya siri.
Maafisa wa forodha walipata gramu 904 za dhahabu yenye thamani ya dola 29,370 ndani sehemu ya nyuma ya siri.
Mwanamume huyo raia wa Sri Lanka mwenye umri wa miaka 45, alikuwa safarini kwenda nchini India, lakini akasimamishwa kwenye uwanja wa kimataifa wa Colombo.
Maafisa wa forodha waliiambia BBC kuwa walimshuku mwanamume huyo kwa sababu alikuwa akiotembea kwa njia isiyo ya kawaida.