MKUU WA HUDUMA YA MAGEREZA AWASAIDIA WAFUNGWA KUTOROKA KATIKA GEREZA LENYE ULINZI MKALI KABLA YA KUFUKUZWA KAZI.

Mkuu wa huduma ya magereza katika mji Buenos Aires Argentina amefutwa kazi baada ya
wafungwa watatu mashuhuri kutoroka kutoka gereza lenye ulinzi mkali siku ya Jumapili.
Gavana wa jimbo hilo , Bi Maria Eugenia Vidal , alisema yeye alichukua hatua hiyo kwa sababu kulikuwa na ushahidi kwamba wafungwa wote walisaidiwa na maafisa wa idara ya magereza kutoroka .
Wafungwa hao Victor Schillaci na kaka wawili Cristian na Martin Lanatta, walikuwa wanatumikia hukumu ya maisha gerezani kwa makosa ya utekaji nyara na mauaji ya wafanyabiashara watatu katika tukio lililohusishwa na mzozo wa madawa ya kulevya mnamo mwaka wa 2008.
Yamkini walitoroka kutoka kwenye gereza lenye ulinzi mkali zaidi wakitumia bunduki bandia kutishia moja wa walinzi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment