RASMI;ANCELOTTI KUMRITHI PEP GUARDIOLA BAYERN MUNICH

nkupamah media

MUNICH.Ujerumani

Kocha wa Bayern Munich ya Ujerumani, Pep Guardiola ataihama klabu hiyo atakapomaliza mkataba wake katika kipindi cha majira ya joto. Bayern Munich imesema leo kuwa Carlo Ancelotti atachukua nafasi yake
kama kocha mpya katika msimu ujao.
Mwenyekiti wa klabu hiyo, Karl-Heinz Rummenigge ameliambia gazeti la kijerumani linalotoka Jumapili, Bild, kwamba wanashukuru kwa yote yaliyofanywa na Guardiola katika klabu hiyo na wana matumaini watapata mafanikio ya pamoja katika msimu huu. PEPAmesema Ancelotti, kocha mwenye mafaniko anajiunga na Bayern Munich na wamejiandaa kufanya naye kazi. Guardiola raia wa Uhispania anayetokea jimbo la Catalonia, alichukua nafasi hiyo kutoka kwa Jupp Heynckes mwaka 2013.
Aliifanikisha Bayern Munich kushinda katika michuano ya Ligi Kuu ya Ujerumani-Bundesliga, Kombe la Shirikisho la Ujerumani, Kombe la Klabu Bingwa barani Ulaya na Kombe la Dunia la FIFA.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment