DAR ES SALAAM
MBUNGE wa Jimbo la Kigoma Mjini,Zitto
Kabwe amesema kuwa atahakikisha wakati wa vikao vya bunge vitakavyoanza
mwakani anaibana Serikali juu ya baadhi ya mambo hasa katika ufafanuzi
juu ya
lililokuwa sakata la Tegeta Escrow.
Zitto kupitia ukurasa wake rasmi wa
Facebook amefichua kuwa atahakikisha anapambana ili suala hilo
linajibiwa kikamilifu na kwamba pesa zote ambazo Serikali inawadai
wamiliki wa mitambo ya IPTL zinarudishwa kwa wananchi
“Juzi nimewasilisha maswali 5
Bungeni ili yajibiwe na Serikali. Swali la kwanza linahusu umiliki wa
IPTL na tshs 8 bilioni tunazowalipa matapeli hao kila mwezi, kwanini
mtambo haujamilikishwa TANESCO na anayejiita mmiliki wa IPTL kukamatwa
na kushtakiwa. Vile vile ni kwanini Benki ya Stanbic haijachukuliwa
hatua kwa kuamuriwa kurudisha Fedha za akaunti ya #TegetaEscrow.
Mambo 2 ( umiliki wa IPTL na kurudisha kwa fedha tshs 320 bilioni) ndio
mambo ya msingi kabisa katika suala zima la #TegetaEscrow. Haya ndio
nitakufa nayo.”
Juzi nimewasilisha maswali 5 Bungeni ili yajibiwe na Serikali. Swali la kwanza linahusu umiliki wa IPTL na tshs 8

0 comments :
Post a Comment