Azam FC yazifuata Simba, Yanga.

Nkupamah media:

Azam FC.
Azam FC imeungana na timu nyingine sita za Ligi Kuu kutinga robo-fainali ya Kombe la FA baada ya jana kuichapa Panone FC mabao 2-1 mjini Moshi.
 
Ikitoka nyuma kwa bao 1-0 dhidi ya wenyeji, timu hiyo ya Chamazi ililamizika kufanya kazi ya ziada kwenye uwanja wenye changamoto ya mashimo wa Ushirika.
 
Kikosi cha Wanalambalamba kilichoanza na nyota wanne wa kigeni; beki wa kati Serge Wawa, kiungo Michael Bolou na washambuliaji Didier Kavumbagu na Allan Wanga kilazimika kusubiri hadi dakika ya 63 kusawazisha bao la dakika ya 48 lilofungwa na beki Godfrey Mbuda.
 
Beki wa kimataifa kutoka Ivory Coast, Wawa ndiye aliyefufua matumaini ya Azam FC akifuta makosa ya safu ya ulinzi kwa kumalizia kwa kichwa cha kuparaza mpira wa kona iliyopigwa na beki pembeni kulia, Erasto Nyoni kutoka kusini mashariki mwa Uwanja wa Ushirika.
 
Nyoni alipiga kona nyingine murua katika dakika ya 77 ambayo iliwababatiza mabeki wa Panone FC kabla ya kukwamishwa nyavuni kwa shuti 'mtoto' la mguu wa kulia na straika Mkenya, Wanga.
 
Kwa ushindi huo, Azam imeunga na timu sita za Ligi Kuu - Coastal Union, Ndanda, Prisons, Mwadui, Simba na Yanga pamoja na timu pekee ya Ligi Daraja la Kwanza, Geita Gold kukamilisha orodha ya timu nane zitakazochuana kwenye hatua ya robo-fainali
 
Bingwa bingwa wa michuano hiyo ambaye ataiwakilisha Tanzania Bara katika Kombe la Shirikisho barani Afrika mwakani.
 
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment