Malinzi ang'aka upangaji wa matokeo.

Nkupamah media:

Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi
Sakata la upangaji matokeo Ligi Daraja la Kwanza Kundi C, limezidi kuchochea kasi, huku Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi akilazimika kutumia lugha kali dhidi ya waandishi wa habari kupinga tuhuma za yeye kuhusika.
 
Matokeo hayo ya kupangwa, yalizihusisha Geita Goldmine FC ya Geita iliyoibamiza JKT Kanembwa ya Kigoma mabao 8-0, wakati Polisi Tabora wakiifunga JKT Oljoro ya Arusha mabao 7-0. Mechi hizo zilichezwa Februari 13 mwaka huu. 
 
Bosi Malinzi alikuwa akizungumza na waandishi wa habari jana kwenye Ofisi za TFF kuhusu hatma ya upangaji huo matokeo ambao sasa utajadiliwa na kamati ya nidhamu.
Kabla ya kutoa lugha hiyo kali (tunahifadhi) na isiyozoeleka kwake, Malinzi aliulizwa swali: “Katika suala hili la Geita, unatajwa kuhusika na upangaji matokeo na ulikuwa ukifanya mawasiliano na viongozi wa timu mojawapo?.”
 
Akijibu tuhuma hizo, bosi Malinzi aliwaka na kutoa matamshi makali, ambayo yalisababisha pia mkutano kuvunjika.
 
"Naendesha taasisi kubwa kama hii, ninawezaje kuhusika na suala la kupanga matokeo?,” alifoka Malinzi na kuongeza:
“Kama nahusika na kuna mtu ana ushahidi, aende polisi hata leo hii kufungua mashtaka. Kuna mchezo unachezwa hapa, ninajua kila kinachoendelea na wote nawafahamu.”
 
Alisema tangu kumalizika mechi hizo mbili, yeye binafsi na TFF wamekumbana na matamshi ya shutuma.
“Nimekaa kimya kwa sababu suala hili liko mikononi mwa vyombo husika kufanya uchunguzi na kutoa uamuzi.
"Nimetukanwa sana kwenye mtandao wa Jamii forum, redioni, facebook. Nafahamu zilikoanzia shutuma hizi, lakini niwahakikishie watu hao kuwa hawatafika kokote.”
 
Hata hivyo, Malinzi alisema TFF imebaini kuwapo viashiria vya upangaji matokeo kwenye mechi hizo na wahusika wanatarajiwa kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria Machi 20 mwaka huu.
 
Alisema Sekretarieti ya TFF inaandaa mashtaka kuhusiana na kesi hiyo na wahusika wote watajulishwa.
“Jambo hili ni kubwa sana na baada ya kuona kanuni kwenye Kamati ya Mashindano hazijitoshelezi, tumeamua kulipeleka Kamati ya Nidhamu.
 
"Siku zote Fifa, Caf, TFF zinapiga vita upangaji wa matokeo, katika hili TFF ni walalamikaji na tutaeleza ya kwetu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment