Ukishangaa Y a Musa Utayaona Ya ?...........Sokwe Ajifungua Kwa Upasuaji.

Nkupamah media:


Sokwe amezalishwa kwa upasuaji wa dharura kusini Magharibi mwa Uingereza katika sehemu uliyotengwa kwa kuhifadhia wanyama inayojulikana kama Bristol Zoo.

Mama na mtoto wa sokwe huyo wanaendelea vyema ,sokwe huyo alizaliwa kupitia upasuaji usio wa kawaida baada ya mama yake kuonyesha ishara za ugonjwa hatari wa shinikizo la damu.
Jopo la kuongoza shughuli ya upasuaji kwa sokwe huyo liliongozwa na Profesa David Cahill aliyeitwa kutoka hospitali ya kina mama NHS na mtoto wa kike alizaliwa kwa oparesheni hiyo.

Kumekuwa na sokwe wachache waliofanyiwa upasuaji wakati wa kujifungua duniani,kisa cha hivi karibuni kikiwa kile cha San Diego Safari Park mwaka 2014.
Share on Google Plus

About Mng'atuzi blog

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment