GAPCO YAWAPA NEEMA WALEMAVU KATIKA MBIO ZA KILIMANJARO MARATHON 2016


Mshindi wa mbio za Kilometa 10 za Kilimanjaro Marathon 2016, Vosta Peter (30) akishangilia mara baada ya kumaliza. Mbio hizo za Kilometa 10 zilidhaminiwa na kampuni ya GAPCO na kufanyika mjini Kilimanjaro mwishoni mwa wiki iliyopita.
Mshindi wa kwanza kwa mbio za walemavu kilomita 10, Vosta Peter (30) akipokea cheki ya Shilingi Milioni Moja kutoka kwa kampuni ya GAPCO, wanaomkabidhi ni Meya wa Manispaa ya Moshi Raymond Mboya (kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Gapco Afrika Mashariki, Macharia Irungu (anayepiga makofi toka kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa GAPCO Tanzania, Vijay Nair. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
——————————————————————————————–
Habari na Cathbert Kajuna.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya GAPCO Afrika Mashariki, Macharia Irungu amewataka wanamichezo kujibidishe kwa kufanya mazoezi mara kwa mara ili waweze kufanya vizuri katika mashindano wanayoshiriki.
Akizungumza mwishoni mwa wiki mjini Kilimanjaro wakati wa Mashindano ya Kilimanjaro Marathoni 2016, ambapo GAPCO ndiyo waliodhamini upande wa Walemavu, alisema kuwa wanamichezo wengi walemavu na hata wasiowalemavu hujisahau sana kufanya mazoezi ya kutosha jambo linalowafanya wengi wao kutoweza kufanikiwa kushinda kwenye mashindano.
Aliongeza kuwa wao kampuni ya GAPCO waliweza kujitolea kuwasaidia walemavu ili waweze kuonyesha vipaji vyao japo mwanzo waliweza kuwasisitiza wafanye mazoezi na ndiyo maana wameweza kufanya vyema.
“Napenda kuwaasa wanamichezo wale walemavu na wasio walemavu, wapende kujitoa kufanya mazoezi ya kutosha maana siri ya ushindi ni mazoezi wala hakuna muujiza unaoweza kukupa ushindi kama haujajitoa kufanya mazoezi ya kutosha,” alisema Irungu.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya GAPCO Tanzania, Vijay Nair alisema wamefurahishwa na mahudhurio ya watu wenye ulemavu waliojitoa kushiriki mashindano hayo, na wao hawatawatupa wataendelea kuwa nao bega kwa bega.
Bw. Nair aliwaasa walemavu wawe na moyo wa upendo na mshikamano ili waonyeshe mfano bora hata wanapojitokeza kusaidiwa wafaidike kwa pamoja.
Mashindano ya mbio za Kilimanjaro marathon za 10KM kwa walemavu zilidhaminiwa na GAPCO ambapo shindano lilijumuisha baiskeli za walemavu zenye matairi matatu zenye viwango vya kimataifa wapatao 60 kutoka Dar es Salaam, Arusha, Moshi na Zanzibar.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment