LAPF KUKUTANISHA WADAU WAKE MKOANI ARUSHA MACHI 10 NA 11 MWAKA HUU

Nkupamah media:
1
Meneja Masoko na Mawasiliano  wa LAPF, James Mlowe akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wao uliofanyika Milenium Tower jijini Dar es salaam wakati alipoelezea kuhusiana na mkutano wa mwaka wa wadau wa LAPF unaotarajiwa kufanyika  kwenye ukumbi wa AICC mwezi huu kwa sikU mbili  jijini Arusha. Pichani kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Wanachama Bw. Valerian Mablangeti.
2
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia taarifa iliyotolewa na Meneja Masoko na Mawasiliano  wa LAPF, James Mlowe wakati akizungumza nao katika ofisi za Shirika hilo zilizopo Mkumbusho jijini Dar es salaam.
3
Mkurugenzi wa Huduma za Wanachama Bw. Valerian Mablangeti akiwafafanulia jambo waandishi wa habari wakati wa mkutano huo kulia ni Bw. James Mlowe Meneja Masoko na Mawasiliano wa LAPF.
……………………………………………………………………………….. MFUKO wa Pensheni wa LAPF umefanikiwa kuwa na sh.trioni moja  na bilioni 87 za thamani ya uwekezaji kutoka mwezi juni mwaka jana.
Hayo yalibainishwa na Meneja Masoko na Mawasiliano wa LAPF James Mlowe wakati akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi kuhusu mkutano mkuu wa nane wa mfuko huo unaotarajiwa kufanyika Machi 10 na 11 katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC jijini Arusha.
Alisema LAPF imeendelea kupiga hatua kila mwaka ukilinganisha na mifuko mingine ya hifadhi ya jamii hapa nchini.
” LAPF imeweza kutoa mikopo ya masomo kwa watu 800 katika maeneo mbalimbali nchini yenye thami ya sh.bilioni 1.2 jambo ambalo tunajivunia” alisema Mlowe.
Akizungumzia kuhusu mkutano huo, Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa LAPF, Valerian Mablangeti alisema maandalizi ya mkutano huo yamekamilika  kwa wadau wa mfuko huo kupatiwa barua za mualiko.
Alisema mgeni rasmi katika mkutano huo anatarajiwa kuwa  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora, George Simbachawene na kuwa mawaziri wengine wakaoshiriki kwenye mkutano huo ni  Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama na  Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora, Jafo Selemani .
Alisema katika mkutano huo Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali atatoa taarifa ya hesabu za mfuko huo na pia kutakuwa na mada inayohusu afya kutoka kwa Daktari wa  Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH)

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment