Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha
Sheria Tanzania Mhe. Jaji Aloysius Mujulizi (Kushoto) akimkabidhi
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dk. Harison Mwakyembe Taarifa ya Utafiti
wa Sheria ya Ununuzi wa Umma. Wengine pichani ni Katibu wa Wizara ya
Katiba na Sheria Prof. Sufini Mchome (wa pili kulia) na Katibu Mtendaji
wa Tume Bw. Casmir Kyuki.

Mwenyekiti wa Tume Mhe. Jaji
Aloysius Mujulizi akizungumza wakati wa makabidhiano ya Taarifa ya
Utafiti wa Sheria ya Ununuzi wa Umma. Makabidhiano yalifanyika katika
ukumbi wa Wizara ya Katiba na Sheria Dar es Salaam.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.
Dk Harison Mwakyembe akiongea mbele ya waandishi wa habari (hawapo
pichani) wakati wa makabidhiano ya Taarifa ya Utafiti wa Sheria ya
Ununuzi wa Umma.
Katibu Mtendaji wa Tume ya
Kurekebisha Sheria Tanzania Bw. Casmir Kyuki akizungumza wakati wa
makabidhiano ya Taarifa ya Utafiti wa Sheria ya Ununuzi wa Umma.
Katibu wa Wizara ya Katiba na
Sheria Prof. Sifuni Mchome akitoa maelezo mafupi wakati wa makabidhiano
ya Taarifa ya Utafiti wa Sheria ya Ununuzi wa Umma.
Sehemu ya Waandishi wa habari waliohudhuria makabidhiano ya Taarifa ya Utafiti wa Sheria ya Ununuzi wa Umma (Picha zote na Munir Shemweta wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania).
0 comments :
Post a Comment