Mwanafunzi
 wa shule ya SEKONDARI NAMABENGO ambaye hakufahamika jina akionyesha 
kidonda anachouguza kutokana na fimbo ambazo wanapigwa na mwalim mkuu 
msaidizi wa shule hiyo SHAIB CHAMPUNGA.
 Wanafunzi wa shule ya sekondari namabengo wakiwa wamekaa na kumsikiliza afisa elimu wa wilaya hiyo ambaye hayupo pichani .
………………………………………
Na Gidion Mwakanosya.
Wanafuzi
 106 wa kidato cha sita katika shule ya sekondari ya Namabengo wilaya ya
 Namtumbo mkoani Ruvuma wameandamana kwenda kumwona mkuu wa mkoa Said 
Mwambungu kumpelekea malalamiko dhidi ya vitendo vya 
udharirishaji wanavyofanyiwa na makamu mkuu wa shule hiyo Shaibu 
Champunga.
Mwalimu
 huyo anadaiwa kutoa vitisho na lugha za matusi kwa wanafunzi,kuchapwa 
viboko visivyo na idadi,kuingi kwenye bweni la wanafunzi wa
kike nyakati za usiku bila kuongozana na matroni na kuwalazimisha kutaka kufanya mapenzi pamoja na kuwazuia wanafunzi wa kike kulala bwenini.
kike nyakati za usiku bila kuongozana na matroni na kuwalazimisha kutaka kufanya mapenzi pamoja na kuwazuia wanafunzi wa kike kulala bwenini.
Kutokana
 na malalamiko ya wanafunzi hao walitaka kwenda kumwona mkuu wa mkoa ili
 aweze kusikiliza na kuzipatia ufumbuzi kero zao juhudi
za kutaka kuonana na mkuu huyo wa mkoa ziligonga mwamba wakati wamesha tembea kwa miguu kilomita Zaidi ya 16 kabla ya kufikla Songea mjini ambako askari polisi wakiongozwa na mkuu wa polisi wilaya ya Namtumbo kuwazuia wasiendelee na maandamano.
za kutaka kuonana na mkuu huyo wa mkoa ziligonga mwamba wakati wamesha tembea kwa miguu kilomita Zaidi ya 16 kabla ya kufikla Songea mjini ambako askari polisi wakiongozwa na mkuu wa polisi wilaya ya Namtumbo kuwazuia wasiendelee na maandamano.
Wanafunzi
 hao walikutwa kijiji cha Mlete  kilicho nje kidogo ya manispaa ya 
Songea ambapo askari polisi waliwaamuru wasimame ndipo mkuu wa polisi 
wilayani humo aliwataka waeleze sababbu za kufanya maandamano bila 
kibali,wanafunzi hao walimweleza kuwa kila mtu anahaki ya kuongea kwa 
kuwa walishatoa malalamiko yao kwa mkuu wa shule lakini hayakusikilizwa 
hivyo waliona vema wakakutane na mkuu wa mkoa labda ataasikiliza.
Muda
 mfupi baadae alifika katibu tawala wa Namtumbo Alkwine Ndimbo na 
kusikiliza malalamiko mengi ya wanafunzi ambapo walimweleza kuwa
makamu mkuu wa shule ya Sekondari Shaibu Champunga hawamtaki shuleni hapo kwa sababbu anatuhumiwa kuwa na lugha chafu zenye kejeri ikiwa ni pamoja na kuwataja kwa majina wanafunzi wanaodaiwa kuwa na ugonjwa wa Ukimwi.
makamu mkuu wa shule ya Sekondari Shaibu Champunga hawamtaki shuleni hapo kwa sababbu anatuhumiwa kuwa na lugha chafu zenye kejeri ikiwa ni pamoja na kuwataja kwa majina wanafunzi wanaodaiwa kuwa na ugonjwa wa Ukimwi.
Walisisitiza
 kuwa shule hiyo haina miundombinu mizuri ambapo wamedai kuwa vyoo ni 
vibovu havifai kutumika,baadhi ya madarasa hayana sakafu
paja na kwamba wanalazimika kwenda umbali mrefu kufuata maji.
paja na kwamba wanalazimika kwenda umbali mrefu kufuata maji.
Baada
 ya viongozi hao kusikiliza malalamiko ya wanafunzi waliwataka warudi 
shuleni ili wakatoe maamuzi mbele ya wanafunzi wote pamoja na
walimu jambo ambalo wanafunzi walikubali na kusitisha maandamano.
walimu jambo ambalo wanafunzi walikubali na kusitisha maandamano.
Kwa upande wake ofisa elimu wa sekondari wilaya ya Namtumbo Patrick Atanasi ambaye aliyefika kwa kuchelewa wakati tayari katibu tawala wa
 wilaya hiyo Ndimbo ameshakubaliana na wanafunzi warudi shuleni alisema 
kuwa kitendo walichofanya wanafunzi cha kuandamana ni kosa kubwa na 
utovu wa nidhamu na inapaswa kilaaniwe na kuwachimba mkwara wasirudie 
tena jambo lililowafanya wanafunzi kuguna.
Jitihaa
 za kumpata kamanda wa polisi ofisini kwake na kwa njia ya simu hakuzaa 
matunda ili kudhibitisha tukio hilo badala yake alitafutwa
mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai moa wa Ruvuma Levokatus malimi alikili kutokea kwa tukio hilo mbalo alidai kuwa limeshaanza kufanyiwa kazi.
mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai moa wa Ruvuma Levokatus malimi alikili kutokea kwa tukio hilo mbalo alidai kuwa limeshaanza kufanyiwa kazi.




0 comments :
Post a Comment