Donald Trump
Mgombea 
wa urais nchini Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican Donald Trump
 ameahidi kubadilisha sifa zake katika mkutano wa faragha na viongozi wa
 Republican.
Mfanyibishara
 huyo ambaye yuko kifua mbele katika kuwania urais kupitia chama hicho 
alitoa ujumbe wake kupitia wasaidizi wake ,kulingana na chombo cha 
habari cha AP.
Kuimarika
 kwake katika mchujo huo kufikia sasa kumetuma ishara miongoni mwa 
viongozi wa chama hicho kwamba matamshi pamoja na sera zake huenda 
zisiwavutie wapiga kura.
Majimbo matano yanapiga kura siku ya Jumanne kumchagua mgombea wao wa urais.
Bwana 
Trump ana uongozi mkubwa wa idadi ya wajumbe lakini huenda asipate 
wajumbe 1,237 anaohitaji kushinda mchujo huo bila ya mkutano wa 
wanachama.
Wasaidizi wamewaambia viongozi wa chama kwamba amekuwa akibadilisha sifa zake na kwamba hatua hiyo imeanza kufua dafu.

0 comments :
Post a Comment