Serikali
 kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), jana imezifungua ofisi za 
Kampuni maarufu ya uwakili ya Mbunge wa Butiama, Nimrod Mkono, ikiwa ni 
siku chache baada ya kuzifungia kwa madai kuwa kampuni hiyo inadaiwa 
kodi ya shilingi bilioni 1.
TRA
 waliwasili katika jengo la ofisi hizo zilizoko katika jengo la Bank ya 
Exim iliyoko jijini Dar es Salaam (ingawa ilikuwa sikukuu), pamoja na 
Kampuni ya udalali ya Yono na kuzifungua ofisi hizo mbele ya Nimrod 
Mkono na binti yake.
Mkurugenzi
 wa huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA, Richard Kayombo amekiri 
kufunguliwa kwa ofisi hizo. Kayombo amesema kuwa uamuzi huo ulifikiwa 
baada ya kuwepo kwa makubaliano kati ya pande mbili na ahadi ya kufanya 
malipo iliyowekwa na mkono.
“Ni
 kweli muda upo tuliokubaliana lakini hatutaki uwe katika vyombo vya 
habari, kutokana na nia ya dhati aliyoonesha Mkono ndio maana 
tumekubaliana nae,” Kayombo anakaririwa.
Hatua
 hiyo imefikiwa huku kukiwa na taarifa kuwa ingawa Mkono amefungiwa 
ofisi zake akidaiwa kodi ya shilingi bilioni 1, yeye anaidai Serikali 
takribani shilingi bilioni 9 kwa kazi alizofanya ndani ya Tanzania Bara 
na Zanzibar.



Blogger Comment
Facebook Comment