Kufuatia
tuhuma zilizotolewa hivi karibuni na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe.
Paul Makonda zikiwahusisha baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi
kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya, Mkuu wa Jeshi la Polisi
nchini, IGP Ernest Mangu amewasimamisha kazi Askari 12 waliotuhumiwa ili
uchunguzi ufanyike dhidi yao.
Akizungumza
na vyombo vya habari muda mfupi uliopita, IGP Mangu alisema ni lazima
Jeshi la polisi lichukue hatua kali dhidi ya yeyote atakayebainika
kujihusisha na vitendo hivyo, hata kama ni Askari.
"Jeshi
la Polisi linachukua hatua madhubuti za kuwachunguza Askari na Wasanii
wote waliotuhumiwa na baada ya uchunguzi kumamilika hatua za kisheria
zitachukuliwa kwa yeyote atakayethibitika kwa uhalifu huo" alisema IGP Mangu.
Pia
IGP Mangu ameiomba jamii kuendelea kutoa taarifa za uhalifu wa aina
yeyote ili nchi iendelee kuwa salama. Hapo chini ni Majina ya Askari
wanaotuhumiwa kujihusisha na biashara ya Madawa ya kulevya, ambao
wamesimamishwa kazi.
0 comments :
Post a Comment