Wakati Tanzania imejitoa katika Mpango wa Uendeshaji Shughuli za Serikali kwa Uwazi (OGP), sababu za kufanya hivyo zimebainika.
Barua ya Tanzania kujitoa katika mpango huo iliyoandikwa na Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki Kikanda na Kimataifa, Balozi Augustine Mahiga ya Juni 29 iliyowekwa kwenye tovuti ya OGP imeeleza sababu ni kutokana na kuwepo kwa Sheria ya Upatikanaji wa Habari ya mwaka 2016.
Amesema sheria hiyo inalenga kuongeza haki ya upataji wa taarifa na uwazi wa shughuli za Serikali.
Sababu nyingine amesema ni Serikali kuanzisha Tovuti Kuu ya Takwimu Huria (www.opendata.go.tz) kuchapisha data ili zitumiwe na mtu yeyote na hasa kutoka sekta za kipaumbele za elimu, maji na afya.
Pia, amesema Tanzania ni mwanachama wa Mpango wa Afrika wa Kujitathmini Kiutawala Bora (APRM) wenye malengo sawa na OGP.



0 comments :
Post a Comment