@nkupamah blog
Washirika wa pande zote mbili pamoja
na Kikundi cha Sanaa cha Tingatinga wakionyesha baadhi ya kazi za sanaa
watakazokuwa wakishirikiana mbele ya waandishi wa ahabari (hawapo
pichani) wkaati wa utiaji saini wa Mkataba wa makubalianao ya kufanya
kazi pamoja leo katika
Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO).
Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Bwana
Godfrey Mngereza (kushoto) akifafanua jambo wakati wa utiaji saini wa
Mkataba wa makubaliano kati ya Kikundi cha Sanaa cha Tingatinga na
Kampuni ya Kampuni ya Bricoleur Holdings ya nchini Japan. Katikati ni
Wakurugenzi wa Kampuni ya Bricoleur Holdings ya nchini Japan Bwana Shoji
Tsuchiya pamoja na Bi. Yu Shiran.
……………………………………………………………………………………..
Na Tupokigwe Marco na Mwanahamisi Matasi
Chama cha Sanaa cha uchoraji picha maarufu
kama Tinga Tinga kimetiliana saini Mkataba wa Makubaliano wa miaka
mitano wa kufanya kazi kwa pamoja na Kampuni ya Bricoleur Holdings Co.
Ltd ya nchini Japan utakaokiwezesha chama hicho kunufaika kwa kuuza kazi
zake Kimataifa.
Akiongea leo wakati wa utiaji
saini wa Mkataba huo, Mwenyekiti wa Chama cha Sanaa cha Tinga Tinga,
Bwana Zachi Chimwanda ameeleza kuwa, utiaji saini wa Mkataba huo utakua
chachu ya maendeleo katika kuwakomboa wasanii wachoraji katika kipato
chao na kuboresha hali zao za kimaisha kwakuwa kazi zao sasa zitakuwa
zikiuzwa ndani na nje ya nchi.
Kwa upande wake Katibu Mtendaji
wa Baraza la Wasanii la Taifa (BASATA), Bwana Godfrey Mngereza alieleza
kuwa Mkataba waliosaini kati ya Tinga Tinga na watu wa Bricoleur
Holdings Co. Ltd utaimarisha kazi za Wasanii katika fani ya uchoraji
ikiwemo kuongeza vipato vyao.
”Sanaa ni kazi lakini pia ni
biashara, imefika wakati kwa wasanii kufaidika na jasho lao, kampuni hii
watakua wakitafuta masoko kule Japan ili kazi hizi za wachoraji toka
Tanzania ziweze kununuliwa hali ambayo itawaongezea kipato”, alisema
Mngereza.
Aliongeza kuwa Mkataba
uliosainiwa kati ya pande zote mbili umepitia taratibu zote za
kiserikali na Taasisi zinazohusika na mambo ya sanaa na maslahi ya
msanii na msanii yule aliyehusika katika kuchora picha fulani atanufaika
na mkataba huo.
”Kwa msanii atakehusika binafsi
na uchoraji picha mkataba utamwezesha kujua atanufaika vipi na kwa muda
gani”, aliongeza Mngereza.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa
Kampuni ya Bricoleur Holdings Co. Ltd, Bi. Yu Shiran ameeleza kuwa
mpango huo wa Mkataba kati yao na Tingatinga una lengo la kukitangaza
Chama hicho cha wachoraji wa Tanzania Kimataifa.
‘’Kwa kutumia taarifa za
kidijiti za Tingatinga tutaweza kushirikiana na watengenezaji mbalimbali
wa bidhaa, na ili kulithibitisha hili, sisi na Tingatinga tumekuwa
katika mjadala wa takriban mwaka mzima sasa’’, alisema Bi. Shiran.
Tinga Tinga Arts Group
lilianzishwa nchini Tanzanja na Edward Saidi Tingatinga ambaye alifariki
mwaka 1972 ambapo kwa sasa kundi hilo lipo maeneo ya Oysterbay jijini
Dar es Salaam kikijihusisha na sanaa ya uchoraji.


0 comments :
Post a Comment