Mkurugenzi wa Maendeleo ya
Utamaduni Profesa. Hermas Mwansoko akiwa katika picha ya pamoja na
baadhi watumishi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni wakati hafla ya
kumuaga
rasmi Mkurugenzi huyo anayemaliza muda wake jana ofisini kwake.
Mkurugenzi wa maendeleo ya
Utamaduni Profesa. Hermas Mwansoko akizungumza na watumishi wa Idara ya
Maendeleo ya Utamaduni wakati akiwaaga rasmi jana ofisini kwake.
Mkurugenzi huyo anastaafu rasmi kuanzia tarehe 25 Desemba 2015.
Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo
ya Utamaduni sehemu ya Sanaa Bibi. Leaha Kihimbi akielezea jambo wakati
wa hafla ya kumuaga Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni anayemaliza
muda wake Profesa Hermas Mwansoko (kulia) jana jijini Dar es Salaam.
Afisa Utamaduni wa kutoka Wizara
ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Msami akitoa neno kwa niaba
ya watumishi wa Idara ya Utamaduni wakati wa hafla ya kumuaga Mkurugenzi
wa Maendeleo ya Utamaduni anayemaliza muda wake katika utumishi wa umma
Profesa. Hermas Mwansoko jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya watumishi wa Idara ya
Utamaduni wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea wakati
wa hafla ya kumuaga Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni anayemaliza
muda wake katika utumishi wa umma Profesa. Hermas Mwansoko jana jijini
Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa maendeleo ya
Utamaduni Profesa. Hermas Mwansoko akipokea zawadi ya picha inayoonyesha
maisha ya kijijini wakat wa hafla kumugaa jana jijini Dar es
Salaam.anayemkabidhi zawadi hiyo ni Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya
Utamaduni sehemu ya Sanaa Bibi. Leaha Kihimbi . Mkurugenzi huyo
anastaafu rasmi kuanzia tarehe 25 Desemba 2015.


0 comments :
Post a Comment