Hospitali ya Taifa Muhimbili(MNH) inafunga mashine nyingine ya CT- Scan ambayo inategemewa kuanza kutoa huduma kesho mchana.
“Hivyo kufikia jumatatu ijayo
Hospitali hiyo itakua na mashine mbili za CT-Scan ambazo zitakua
zinafanya kazi hatua ambayo itaboresha zaidi utoaji wa huduma kwa
wagonjwa ambao wanatakiwa kupimwa kwa kutumia mashine hiyo,” amesema
Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Watoto na Wazee Ummy
Mwalimu.
Waziri wa Afya , Maendeleo ya
Jamii, Jinsia , Watoto na Wazee Ummy Mwalimu ameyasema hayo leo wakati
alipotembelea mashine za CT-Scan na MRI katika hospitali hiyo.
Pamoja na mambo mengine Waziri
huyo ameshauri ripoti za wagonjwa wanapimwa kwa kwa kutumia mashine
hizo zitolewe haraka ili kuwapunguzia gharama za kukaa muda mrefu
wagonjwa wanaotoka katika mikoa mingine.
Akizungumzia kuhusu mashine ya
CT-Scan na MRI ambazo zimeharibika Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MHN
Profesa Lawrence Mseru amesema juhudi za kutengeneza mashine hizo
zinafanyika na kwamba kifaa cha CT- Scan kilichoharibika kitaingia leo
usiku wakati Spea ya MRI imeshawasili na matengenezo yanaendelea.
Mashine ya CT-Scan hupima wastani wa wagonjwa 40 hadi 60 kwa saa 24 wakati MRI hupima wagonjwa 20 kwa siku.


0 comments :
Post a Comment