Nkupamah media:
Naibu Waziri wa Habari ,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akimkabidhi Mhasibu
wa wizara hiyo Godfrey Osmund shilingi milioni tatu zilizotolewa na mdau
wa michezo ambaye hakutaka jina lake litajwe kwaajili ya kuisaidia
timu ya wanawake ya mpira wa miguu ya Twiga Stars. Fedha hizo zimewekwa
katika Benki ya NMB Bank House akaunti namba “20110001677
inayojulikana kwa jina la Twiga Stars Special Fund”.
Naibu Waziri wa Habari ,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akimsikiliza Mhasibu
wa wizara hiyo Godfrey Osmund mara baada ya kumkabidhi shilingi milioni
tatu zilizotolewa na mdau wa michezo ambaye hakutaka jina lake litajwe
kwaajili ya kuisaidia timu ya wanawake ya mpira wa miguu ya Twiga Stars.
Ijumaa ya wiki hii timu hiyo itacheza na Zimbabwe mashindano ya
awali ya kufuzu kombe la Afrika kwa wanawake.
Naibu Waziri wa Habari ,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akimweleza jambo
Mhasibu wa wizara hiyo Godfrey Osmund mara baada ya kumkabidhi
shilingi milioni tatu zilizotolewa na mdau wa michezo ambaye hakutaka
jina lake litajwe kwaajili ya kuisaidia timu ya wanawake ya mpira wa
miguu ya Twiga Stars. Mhasibu Osmund alizipeleka fedha hizo katika
Benki ya NMB Bank House akaunti namba “20110001677 inayojulikana kwa
jina la Twiga Stars Special Fund”.
Picha na Anna Nkinda
0 comments :
Post a Comment