TOKYO,Japani.
TAMATI ya michuano ya klabu bingwa ya
Dunia inafika leo ambapo kutachezwa mechi mbili fainali,ambapo itaanza
mechi ya kutafuta mshindi wa tatu itakayo chezwa saa nne ya asubuhi kwa
saa za Afrika mashariki na kufuatiwa na mechi ya kutafuta mshindi wa
kwanza na pili.
Hata hivyo macho na maskio ya mashabiki
wengi wa soka dunian yatakuwa katika
mchezo wa fainali ambao utachezwa
majira ya mchana wa saa saba kwa saa za Afrika Mashariki biana ya
mabingwa wa Ulaya,Fc Barcelona na mabingwa wa Amerika kusini River
Plate.
Fc Barcelona huenda leo hii
wakawahusisha wachezaji wao hatari Lionel Messi na Neymar ambao
hawakucheza katika mchezo wa nusu fainali dhidi ya Guangzhou Everbgrande
ya nchini China,
Hata
hivyo nyota wa Barcelona Luis Suarez huenda leo hii akajihakikishia
kutwaa kiatu cha mfungaji bora wa michuano hiyo bara baada ya kuifungia
timu yake magoli matatu katika mchezo wa nusu fainali.


0 comments :
Post a Comment