BBC
Aina
mpya ya rangi ambayo imeundwa kwa mtindo maalum ili kurejesha mkojo kwa
anayejaribu kuukojolea ukuta uliopakwa rangi hiyo, imeanza kujaribiwa na
manispaa moja jijini London.
Rangi hiyo ya majimaji itakuwa ikipakwa
katika maeneo maarufu kwa wanywaji pombe, katika tarafa za
Shoreditch na
Dalston, mashariki mwa London.
Manispaa ya Hackney, imesema imekuwa
ikitumia £100,000 kusafisha mkojo kutoka katika kuta za manispaa hiyo na
pembezoni mwa barabara, mahala ambapo watu huenda haja ndogo ovyo.
Feryal Dermici, ambaye ni mbunge wa
manispaa hiyo anasema: “ikiwa hatua ya kuwapiga faini haiwazuii kukojoa
ovyo barabarani na pembezoni mwa njia, sasa hatari ya kumwagikiwa na
mkojo wao wenyewe, litakuwa jambo la busara”.
Sasa, adhabu ni kujenga kizuizi
itakayopakwa rangi ambayo itawezesha mkojo kumrudia mkojoaji, ili
anapomwagikiwa na mkojo wake mwenyewe, basi atapata adhabu inayomfaa.
Pia lengo jingine ni kuzuia mkojo kulowesha ukuta, kuondoa madoadoa ya uchafu na uvundo.
Haijafichuliwa hasa maeneo ambayo itapakwa rangi hiyo, ili wanaoenda haja wasijue na kukwepa maeneo hayo pekee.


0 comments :
Post a Comment