NHIF yaridhishwa na matumizi ya mikopo

mic2
Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa Bw. Michael Muhando akikabidhi vifaa tiba kama vile Ultra Sound, Incubator, Mashine ya dawa za Usingizi ,Vitanda vya Kujifungulia na Kadhalika kwa Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya mkoa wa Singida  Pendaeli Maasay leo
mkoani humo
mic3
Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa Bw. Michael Muhando akiangalia vifaa tiba mbalimbali vilivyotolewa na mfuko huo kwa hospitali ya Mkoa wa Singida.
mic4
Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa Bw. Michael Muhando akimuonyesha vifaa tiba vilivyokabidhiwa Kaimu  Mganga Mkuu wa hospitali ya mkoa wa Singida Dkt. Ernest Mugeta na kushoto ni Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya mkoa wa Singida  Pendaeli Maasay
mic5
Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa Bw. Michael Muhando akimuonyesha vifaa tiba   Kaimu  Mganga Mkuu wa hospitali ya mkoa wa Singida Dkt. Ernest Mugeta.
…………………………………………………………………………………..
  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya  NHIF Bwana Michael Mhando ameelezea kuridhishwa na matumizi ya mkopo uliotolewa kwa Hospitali ya mkao wa Singida.
Hospitali hiyo ilichukua mkopo wa Shilingi Milioni Mia Tano kutoka NHIF kwa ajili ya Ununuzi wa vifaa Tiba vya hospitali hiyo. Akizungumza baada ya kukagua vifaa hivyo Bwana Mhando  baada ya amesema ameridhiswa na matumizi ya mkopo huo kwani umefanya kazi iliyokusudiwa. 
Amesema NHIF  itaendelea kushirikiana na uongozi wa mkoa huo ili kuboresha huduma za matibabu kwa wanachama wa NHIF na wananchi kwa ujumla.
Aidha amewahimiza watoa huduma wengine kuendelea kuchukua mikopo ili kuboresha huduma ktk vituo vyao vya matibabu. Hivi sasa Mfuko huo umeanza pia kutoa mikopo ya dawa ili kukabiiliana na uhaba wa dawa ktk vituo vya matibabu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment