Wednesday, December 2, 2015
 
@nkupamah blog
Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda, amesema ameridhishwa na kasi ya utendaji kazi ambayo Rais Dk. John Magufuli na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim, wameanza nayo na kwamba ana imani kwa uchapakazi na uadilifu wao, wataivusha Tanzania na kuifikisha kwenye uchumi wa kati ambako serikali imejielekeza kufika.
Pinda
 amesema yeye anaona kasi hiyo ya utendaji inayochukuliwa na serikali ya
 awamu ya tano, ni sahihi na kinachohitajika ni kumuombea tu kwa Mungu.
Alitoa
 kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana baada ya kufungua Kituo cha 
Utamaduni cha China hapa nchini katika mahojiano maalum na waandishi wa 
habari waliotaka kufahamu namna anavyoona kasi ya utendaji wa Serikali 
ya Awamu ya Tano.
Alisema
 kila rais anayeingia madarakani, lazima aingie na nguvu yake ya kufanya
 kazi ambayo inaweza kujenga imani kwa wananchi wake na yeye anaona sawa
 kasi hiyo aliyoingia nayo Dk. Magufuli.
“Unajua
 kila rais anayeingia madarakani, lazima aje na nguvu yake ambayo 
itajenga imani kwa wananchi, hivyo mimi naona ni sawa tu, kikubwa ni 
kumuombea tu,” alisema Pinda kwa ufupi.



0 comments :
Post a Comment