NAIBU Katibu Mkuu wa CCM (Bara),
Rajab Luhwavi, akisalimiana na viongozi wa CCM mkoa wa Mbeya baada ya
kuwasili mkoani hapa, leo, Machi 31, 2016, kuanza ziara ya kikazi.
Kutoka kushoto ni Katibu wa CCM mkoa wa Mbeya Mwangwi Kundya, Katibu wa
CCM, Wilaya ya Mbeya Vijijini, Lobe Zongo na Katibu msaidizi Mkuu wa
mkoa, Adallah Mayomba.
Naibu
Katibu Mkuu wa CCM, Bara Rajab Luhwai akiwa na mwenyeji wake, Katibu wa
CCM mkoa wa Mbeya, Mwangwi Kundya (kushoto), baada ya kuwasili Uwanja
wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe kwa ajili ya kuanza ziara ya kikazi
mkoani Mbeya.
VIKUNDI VYA WAJASIRIAMALI MKURANGA VYASHAURIWA KUWA KATIKA MWAMVULI WA VICOBA ILI KUPATA SIFA YA KUKOPESHWA
Mkurugenzi
wa Baraza la Uwezeshaji la Taifa, Bengi Issa mwenye kilemba,
akizungumza kwenye kikao cha pamoja na Mbunge wa Mkuranga, Mheshimiwa
Abdallah Ulega kushoto kwake kwa ajili ya kuangalia namna ya
kushirikiana naye kuwasaidia na kuwawezesha wananchi wa Mkuranga. Mbunge Mkuranga asaka uwezeshwaji wa wananchi wake
…………………………………………………………………………………………………………………..
Na Mwandishi
Wetu, Dar es Salaam
Wetu, Dar es Salaam
MBUNGE
wa Jimbo la Mkuranga, wilayani Mkuranga, mkoani Pwani, Abdallah Ulega,
jana amefanya kikao na Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji
Taifa (NEEC), Bengi Issa, kwa ajili ya kutafuta fursa ya
kuwawezesha wananchi wilayani humo.
Mbunge
wa Mkuranga, Mheshimiwa Abdallah Ulega, akizungumza jambo katika kikao
cha pamoja na Mkurugenzi wa Baraza la Uwezeshaji la Taifa (NEEC), Bengi
Issa, hayupo pichani.
Kikao
hicho pia kilihusisha Mkurugenzi wa Uwezeshaji, Afisa Maendeleo ya
Jamii Mkuranga, ambapo pamoja na mambo mengine, kilijadili namna
ya kusaidia vikundi vilivyosajiliwa 285, vikundi vya vicoba 109,
ufugaji wa nyuki, vikundi vya wanawake, vijana na waendesha bodaboda.
Akizungumza
baada ya kikao hicho kumalizika, Ulega aliyewahi pia kuwa Mkuu wa
wilaya Kilwa, alisema kwamba lengo ni kuona wanananchi wa Mkuranga
wanapiga hatua kutoka kwenye hali ya ukata na kufikia kiwango kizuri,
sanjari na kufanikisha maendeleo kwa wananchi wote.
Alisema
kwamba kikao hicho kimemalizika kwa mafanikio ambapo ilishauriwa
kuwa vikundi vya kukopeshana (VICOBA) inabidi viwekwe chini ya
mwamvuli mmoja utakaoviwakilisha vyote.
“Hili litakapofanyika,
Benki ya Posta Tanzania ina utaratibu wa kutoa mikopo ya riba ndogo
kupitia mwamvuli huo unaowakilisha vikundi vyote kwa pamoja, tukiamini
kuwa itasaidia kwa kiasi kikubwa kufanikisha ndoto zetu.
“Lengo
letu ni kuhakikisha kwamba tunaiweka Mkuranga katika kiwango
kizuri ukizingatia kwamba wilaya hii ipo karibu na jiji la Dar es
Salaam, hivyo inaweza kukua kwa kasi kwa sababu mtu anaweza kuishi
Mkuranga na akafanya kazi au kuingia na kutoka kwa urahisi wilayani
kwetu,” alisema.
Aidha
imeshauriwa pia kuanzisha SACCOS ya wafugaji wa nyuki ili kurahisisha
upatikanaji wa mikopo ya vifaa kwa ajili ya ufugaji wa kisasa wa nyuki,
ambapo wana vikundi wanatakiwa kuandaa mpango kazi wao utakaopelekwa
Benki ya Maendeleo kwa ajili ya mkopo, ikiwa na lengo la kuhifadhi
misitu na kuacha utafutaji wa kipato kwa njia ya kukata miti ili
kuzalisha mkaa.
0 comments :
Post a Comment